16 October 2019

Mbeya boy X Dizasta vina X shaolin seneta _ Hasi na chanya lyrics



                Mbeya boy

Napiga taya vibao stair ngumi chek mitindo, mapigo mabaya wote wako chini ya ulingo/

Nilivyosugu demu gani wakunivunja shingo, mistari tindo wako chini ya ukingo/

Nikisimama sioni mdada wakutamba, uliza wenzako nilichomfanya sholi mwamba/

Bila nguvu porini navuta kitu, moshi mwingi kama nachoma msitu/

Nazika marapa walijua mazishi, nilivyo kaligraph yo wakajua madishi/

Kichwani raga maphy nabugi nipo rumba, rip yangu kama choo kwaiyo nipo kila nyumba/

Cheza kibaiskel si unamiguu ya peda, mi nagonga demu yeyote hata akae kwenye zebra/

Rhymes sio matusi ila zinawachanganya, mfano we sio hesabu na nina uwezo wa kukufanya/

                      [Hook]

Mwalimu wa rap nakupa hesabu fanya, chukua hasi weka plus pata jibu gawanya/

Hapo inakua nini (hasi na chanya)x2

                    Dizasta vina

Eyo ticha nimesimama hayashime, natisha napo shika mic kama masai kashika sime/

Nawasha washa sasa imewaka nani azime, naokota tanga naua mwanza zika tarime/

Push rythems kama mjani man wanaelewa, mi na rap sana na ni kama dhambi niliyopewa/

Flani na flani wanaelewa hawataki tu kusema, sauti hewani mitaani sionekana kama hewa/

Dizasta vina ndio future yako, ni kijogoo uliyemkwepa mtaani halafu ukamkuta kwako....Mimi kama kumbukumbu ya torati, kutoka walawi, mwanzo, ayubu yohana, luka marko/

Kudadadeki hamnipi taji homie, maana huu ujio ni kama ford au bogi au radi homie/

Niko kitambo na sihitaji hodi, na wala sipingwi ka zinavyopingwa itikadi za kibabiloni/

Aah na mnapata uhondo nakili, mjeda nazalisha rhythms kama uoto wa asili/

Najua sana mwana inakupasa ukasome, hii waswahili wanaita mwana ukome/ dizasta

Mwalimu wa rap nakupa hesabu fanya, chukua hasi weka plus pata jibu gawanya/

Hapo inakua nini (hasi na chanya)x2

                     Shaolin seneta

Wananihoji eti hatari ni nini, njoo kwenye kiki ndio utajua hatari ni mimi/

Nikichana sina woga ila nawapa pressure, mpaka ma model na wanajiuliza wapi nimetoka/

Wabongo wananita black eminem, sifanyi soft wana wanajua nafanya black game/

Usinivute shati nyakati za mashaka, nina chale mwili mzima mcee utanichana wapi?/

Shaolin kisima cha verse kwa sasa, unaweza nita tajiri wa verse za mada/

y.o.u.n.g hauna swaga, ndani ya uwanja niko moto mpaka messi namanga/

Iwe kwa nguvu ya bia, au soda huwezi nidondosha nimesimama kama zakaria/

Matozi wana shine kwa kuazima, Hii ngoma ni nzito unaweza ukakonda ukiipima/

Mitaani wengi wananiogopa kama kifuku, adhabu kali ni kuweza kuicheza hii ngoma kiduku/

Nadhani kwa heshima na hasira, nikiona matozi wanachana truck bila vina/

                                           [Hook]

Mwalimu wa rap nakupa hesabu fanya, chukua hasi weka plus pata jibu gawanya/

Hapo inakua nini (hasi na chanya)x2