sonunigam
16 October 2019
Mbeya boy X Dizasta vina X shaolin seneta _ Hasi na chanya lyrics
Mbeya boy
Napiga taya vibao stair ngumi chek mitindo, mapigo mabaya wote wako chini ya ulingo/
Nilivyosugu demu gani wakunivunja shingo, mistari tindo wako chini ya ukingo/
Nikisimama sioni mdada wakutamba, uliza wenzako nilichomfanya sholi mwamba/
Bila nguvu porini navuta kitu, moshi mwingi kama nachoma msitu/
Nazika marapa walijua mazishi, nilivyo kaligraph yo wakajua madishi/
Kichwani raga maphy nabugi nipo rumba, rip yangu kama choo kwaiyo nipo kila nyumba/
Cheza kibaiskel si unamiguu ya peda, mi nagonga demu yeyote hata akae kwenye zebra/
Rhymes sio matusi ila zinawachanganya, mfano we sio hesabu na nina uwezo wa kukufanya/
[Hook]
Mwalimu wa rap nakupa hesabu fanya, chukua hasi weka plus pata jibu gawanya/
Hapo inakua nini (hasi na chanya)x2
Dizasta vina
Eyo ticha nimesimama hayashime, natisha napo shika mic kama masai kashika sime/
Nawasha washa sasa imewaka nani azime, naokota tanga naua mwanza zika tarime/
Push rythems kama mjani man wanaelewa, mi na rap sana na ni kama dhambi niliyopewa/
Flani na flani wanaelewa hawataki tu kusema, sauti hewani mitaani sionekana kama hewa/
Dizasta vina ndio future yako, ni kijogoo uliyemkwepa mtaani halafu ukamkuta kwako....Mimi kama kumbukumbu ya torati, kutoka walawi, mwanzo, ayubu yohana, luka marko/
Kudadadeki hamnipi taji homie, maana huu ujio ni kama ford au bogi au radi homie/
Niko kitambo na sihitaji hodi, na wala sipingwi ka zinavyopingwa itikadi za kibabiloni/
Aah na mnapata uhondo nakili, mjeda nazalisha rhythms kama uoto wa asili/
Najua sana mwana inakupasa ukasome, hii waswahili wanaita mwana ukome/ dizasta
Mwalimu wa rap nakupa hesabu fanya, chukua hasi weka plus pata jibu gawanya/
Hapo inakua nini (hasi na chanya)x2
Shaolin seneta
Wananihoji eti hatari ni nini, njoo kwenye kiki ndio utajua hatari ni mimi/
Nikichana sina woga ila nawapa pressure, mpaka ma model na wanajiuliza wapi nimetoka/
Wabongo wananita black eminem, sifanyi soft wana wanajua nafanya black game/
Usinivute shati nyakati za mashaka, nina chale mwili mzima mcee utanichana wapi?/
Shaolin kisima cha verse kwa sasa, unaweza nita tajiri wa verse za mada/
y.o.u.n.g hauna swaga, ndani ya uwanja niko moto mpaka messi namanga/
Iwe kwa nguvu ya bia, au soda huwezi nidondosha nimesimama kama zakaria/
Matozi wana shine kwa kuazima, Hii ngoma ni nzito unaweza ukakonda ukiipima/
Mitaani wengi wananiogopa kama kifuku, adhabu kali ni kuweza kuicheza hii ngoma kiduku/
Nadhani kwa heshima na hasira, nikiona matozi wanachana truck bila vina/
[Hook]
Mwalimu wa rap nakupa hesabu fanya, chukua hasi weka plus pata jibu gawanya/
Hapo inakua nini (hasi na chanya)x2
22 March 2019
MAUAJI YA KIJASUSI YALIYOACHA MASWALI MENGI
Wakuu habari za mchana, natumaini wote wazima. Juzi nilikuwa nasoma kitabu kimoja cha kuhusu mambo ya kijasusi cha "spies against armaggedon" humo nikakutana na term inaitwa DARK ARTS na katika kusaka maana zaidi mitandaoni nikakutana na case moja ya jasusi Gareth williams ambaye kifo chake kilihitimishwa kwa kusema aliuawa na mtu ambaye ni mtaalamu wa "dark arts" sasa kupitia case hii nategemea wajuzi wa hizi mambo mtusaidie je dark arts ni nini hasa kwenye tasnia ya ujasusi.
Tarehe 23 august polisi wa nchini uingereza walikuta mwili wa kijana kwenye kibegi kidogo cha kubebea nguo ndani ya bafu ambaye baadae mwili huo ulitambulika kuwa ni wa Gareth williams ambaye alikuwa anafanya kazi katika shirika la ujasusi la uingereza SIS (MI-6) katika kitengo cha mawasiliano. Kifo hichi kiliacha utata na maswali mengi kwa polisi kwa jinsi tukio hili lilivyotokea hadi kupelekea kifo cha jasusi huyu.
WILLIAMS NI NANI?
Gareth Williams alizaliwa
mwaka 1978 nchini wales iliyomo ndani ya United kingdom, na alikuwa "kipanga" wa hesabu ambapo aliisoma kwenye chuo kikuu cha Bangor na kuhitimu kwa mean GPA ya 1st class akiwa na miaka 17 tu!! Na aliendelea na masomo hayo hadi ngazi ya PhD na baadae kuajirwa katika taasisi ya kijasusi ya mawasiliano (GCHQ) ambapo baadae aliongezewa na majukumu ya ujasusi kupitia shirika la SIS maarufu kama Mi-6 ambalo jukumu lake kubwa ni kukusanya taarifa za kiintelijensia nje ya uingereza.Kazi kubwa ya bwana williams ilikuwa kulinda mifumo ya mawasiliano ya shirika la ujasusi na serikali ya uingereza huku pia akifuatilia mitandao ya watakatishaji pesa duniani
KIFO CHAKE
Baada ya kutoonekana kwa masiku kadhaa, marafiki waliwajulisha police kuhusu hofu yao hivyo mchana wa 23, august 2010 police walienda kukagua nyumba aliyopanga bwana williams. Walipofika walikuta mlango umerudishiwa vizuri, vitu vipo organized, ila hawakumuona na walipofika bafuni wakakutana na kibegi cha aina hii
Walipofungua wakakutana na mwili wa Bwana williamson ambao ulikwisha anza kuoza na katika uchunguzi huo wa awali hawakukuta alama yeyote ya kuumia,kupigwa au kunyweshwa sumu ambayo ingeweza pelekea kifo chake.
Pia wakiwa hapo bafuni hawakuona alama ya vidole vyake au vya mwingine yeyote kwenye kitu chochote ndani ya bafu au apartment hiyo hapo ndipo utata ulipoanza.
UTATA KWENYE UCHUNGUZI
1.Mwili wa williamson ulikutwa kwenye kibegi kidogo cha kubebea nguo ajabu ni kwamba funguo ilikutwa ndani ya begi kwenye mgongo wa william na pia zipu ilifungwa vizuri na kufuli na ushahidi wote unaonyesha zipu ilifungiwa kwa ndani ila bado hakukuwa na alama ya vidole ya williams na wala hakuwa amevaa gloves je iliwezaje kufungwa kwa ndani ilihali kufuli ipo nje na funguo ipo ndani??
2. Nyumba waliikuta haijachezewa kokote sio dirisha sio mlango sio bafu yaani kilakitu kilikuwa kwenye mpangilio wake hivyo kama kuna muuaji basi mlango ungevunjwa au dirisha ila baada ya uchunguzi ikaonekana hakuna sehemu yoyote ya kuingia "iliyochezewa"
3. Pia CCTV camera zilizokuwepo hapo hazikuonyesha mtu akiingia wala akitoka katika makazi hayo ikimaanisha alijiua mwenyewe.
LAKINI.....
4. Baada ya kuanza uchunguzi kama alijiua walishangaa kukuta mwili wake haukuwa na dalili ya sumu yeyote kwenye mwili wake au damu wala jasusi huyo kuishiwa hewa kabla ya kifo hivyo swali likaibuka je alijiuaje??
5. Wachunguzi wakahisi itakuwa alipoingia kwenye begi alishindwa kujitoa hivyo aliishiwa hewa au alipata "ajali" nyingine akafariki lakini walipojaribu kuingia kwenye begi kwa kutafuta ''mtaalam'' wa gymnastics ambaye ana asili ya mwili kama wa williams bado ilikuwa ngumu kufunga begi kutokea ndani hivyo lazima alikuwepo mtu wa pili ambaye alilifunga!!
ILA......
Kama mtu wa pili alimuingiza akiwa hai polisi hawakuona dalili ya williams kupambana kuokoa uhai wake kabla ya kufariki ndani ya begi na wala hawakuona alama ya mikono kwenye zipu upande wa ndani wa begi!!
Hivyo kama kuna mtu alimuua je alimuua kutumia nni?? Hawakuona sumu kwenye damu wala kovu wala ushahidi kwamba alipigwa na kitu kilichopelekea kifo?? Je hapa nini kilimuua??
TAARIFA MPYA YAIBUKA
Ilipofika mwaka 2015 alitokea jasusi wa kirusi ambaye alidai kuna majasusi wenzake wa kirusi walimuua Bwana williams kwa kumuingizia sumu kwenye sikio, lakini taarifa za Bwana huyu zilikosa ushahidi kabisa katika uchunguzi wa polisi na wataalamu wengine wa Mi-6 ukizingatia huyu jasusi alikuwa amekimbia urusi huku uingereza ikikataa kumchukua kwenye shirika lake la kijasusi wakiamini ni pandikizi hivyo taarifa zake zilipuuzwa maana walihisi anatafuta "kiki" ya kuaminika na kuingizwa kwenye shirika lao.
HITIMISHO
Ni kweli majasusi huwa wanatumia taaluma nyingi hata nyingine za kiroho maana kuna story za jasusi mmoja wa kiyahudi huko ufaransa aliyekuwa akipita mtaani ni kma upepo yaani hakuna anayejua kuwa kuna mtu kapita dakika hiyo na wala kwenye CCTV humuoni..... Sasa cha kujiuliza je dark arts inahusisha nguvu zingine za kiroho au ni mafunzo tu ya kiakili na kimwili ya hali ya juu ili kufanya kazi hizi za ujasusi kwa weledi?
Tarehe 23 august polisi wa nchini uingereza walikuta mwili wa kijana kwenye kibegi kidogo cha kubebea nguo ndani ya bafu ambaye baadae mwili huo ulitambulika kuwa ni wa Gareth williams ambaye alikuwa anafanya kazi katika shirika la ujasusi la uingereza SIS (MI-6) katika kitengo cha mawasiliano. Kifo hichi kiliacha utata na maswali mengi kwa polisi kwa jinsi tukio hili lilivyotokea hadi kupelekea kifo cha jasusi huyu.
WILLIAMS NI NANI?
Gareth Williams alizaliwa
mwaka 1978 nchini wales iliyomo ndani ya United kingdom, na alikuwa "kipanga" wa hesabu ambapo aliisoma kwenye chuo kikuu cha Bangor na kuhitimu kwa mean GPA ya 1st class akiwa na miaka 17 tu!! Na aliendelea na masomo hayo hadi ngazi ya PhD na baadae kuajirwa katika taasisi ya kijasusi ya mawasiliano (GCHQ) ambapo baadae aliongezewa na majukumu ya ujasusi kupitia shirika la SIS maarufu kama Mi-6 ambalo jukumu lake kubwa ni kukusanya taarifa za kiintelijensia nje ya uingereza.Kazi kubwa ya bwana williams ilikuwa kulinda mifumo ya mawasiliano ya shirika la ujasusi na serikali ya uingereza huku pia akifuatilia mitandao ya watakatishaji pesa duniani
KIFO CHAKE
Baada ya kutoonekana kwa masiku kadhaa, marafiki waliwajulisha police kuhusu hofu yao hivyo mchana wa 23, august 2010 police walienda kukagua nyumba aliyopanga bwana williams. Walipofika walikuta mlango umerudishiwa vizuri, vitu vipo organized, ila hawakumuona na walipofika bafuni wakakutana na kibegi cha aina hii
Walipofungua wakakutana na mwili wa Bwana williamson ambao ulikwisha anza kuoza na katika uchunguzi huo wa awali hawakukuta alama yeyote ya kuumia,kupigwa au kunyweshwa sumu ambayo ingeweza pelekea kifo chake.
Pia wakiwa hapo bafuni hawakuona alama ya vidole vyake au vya mwingine yeyote kwenye kitu chochote ndani ya bafu au apartment hiyo hapo ndipo utata ulipoanza.
UTATA KWENYE UCHUNGUZI
1.Mwili wa williamson ulikutwa kwenye kibegi kidogo cha kubebea nguo ajabu ni kwamba funguo ilikutwa ndani ya begi kwenye mgongo wa william na pia zipu ilifungwa vizuri na kufuli na ushahidi wote unaonyesha zipu ilifungiwa kwa ndani ila bado hakukuwa na alama ya vidole ya williams na wala hakuwa amevaa gloves je iliwezaje kufungwa kwa ndani ilihali kufuli ipo nje na funguo ipo ndani??
2. Nyumba waliikuta haijachezewa kokote sio dirisha sio mlango sio bafu yaani kilakitu kilikuwa kwenye mpangilio wake hivyo kama kuna muuaji basi mlango ungevunjwa au dirisha ila baada ya uchunguzi ikaonekana hakuna sehemu yoyote ya kuingia "iliyochezewa"
3. Pia CCTV camera zilizokuwepo hapo hazikuonyesha mtu akiingia wala akitoka katika makazi hayo ikimaanisha alijiua mwenyewe.
LAKINI.....
4. Baada ya kuanza uchunguzi kama alijiua walishangaa kukuta mwili wake haukuwa na dalili ya sumu yeyote kwenye mwili wake au damu wala jasusi huyo kuishiwa hewa kabla ya kifo hivyo swali likaibuka je alijiuaje??
5. Wachunguzi wakahisi itakuwa alipoingia kwenye begi alishindwa kujitoa hivyo aliishiwa hewa au alipata "ajali" nyingine akafariki lakini walipojaribu kuingia kwenye begi kwa kutafuta ''mtaalam'' wa gymnastics ambaye ana asili ya mwili kama wa williams bado ilikuwa ngumu kufunga begi kutokea ndani hivyo lazima alikuwepo mtu wa pili ambaye alilifunga!!
ILA......
Kama mtu wa pili alimuingiza akiwa hai polisi hawakuona dalili ya williams kupambana kuokoa uhai wake kabla ya kufariki ndani ya begi na wala hawakuona alama ya mikono kwenye zipu upande wa ndani wa begi!!
Hivyo kama kuna mtu alimuua je alimuua kutumia nni?? Hawakuona sumu kwenye damu wala kovu wala ushahidi kwamba alipigwa na kitu kilichopelekea kifo?? Je hapa nini kilimuua??
TAARIFA MPYA YAIBUKA
Ilipofika mwaka 2015 alitokea jasusi wa kirusi ambaye alidai kuna majasusi wenzake wa kirusi walimuua Bwana williams kwa kumuingizia sumu kwenye sikio, lakini taarifa za Bwana huyu zilikosa ushahidi kabisa katika uchunguzi wa polisi na wataalamu wengine wa Mi-6 ukizingatia huyu jasusi alikuwa amekimbia urusi huku uingereza ikikataa kumchukua kwenye shirika lake la kijasusi wakiamini ni pandikizi hivyo taarifa zake zilipuuzwa maana walihisi anatafuta "kiki" ya kuaminika na kuingizwa kwenye shirika lao.
HITIMISHO
Ni kweli majasusi huwa wanatumia taaluma nyingi hata nyingine za kiroho maana kuna story za jasusi mmoja wa kiyahudi huko ufaransa aliyekuwa akipita mtaani ni kma upepo yaani hakuna anayejua kuwa kuna mtu kapita dakika hiyo na wala kwenye CCTV humuoni..... Sasa cha kujiuliza je dark arts inahusisha nguvu zingine za kiroho au ni mafunzo tu ya kiakili na kimwili ya hali ya juu ili kufanya kazi hizi za ujasusi kwa weledi?
15 March 2019
MJUE MZEE VANGA NA MAAJABU YAKE


Vangelia Gushterova - Vanga, alizaliwa tarehe 31 Mwezi wa Kwanza mwaka 1911 katika mji wa Strumica huko nchini Yugoslavia.
Akiwa na umri wa miaka 3, mama yake alifariki na pia baba yake alienda kupigana mstari wa mbele kwenye vita ya kwanza ya dunia, jambo lililomfanya Baba Vanga kubaki peke yake bila muangalizi.
Akiwa na umri wa miaka 7, baba yake alioa tena hivyo Vanga akapata mama mpya.
Mwaka 1923, familia yao ilihamia Novo Selo, huko Vanga aliishi maisha ya tabu na mateso sana.
Siku moja Vanga akiwa na binamu zake walienda tembelea chemi chem zijulikanazo kama Khan, wakiwa huko kulitokea kimbunga kikali sana ambacho kilomsomba Vanga na kwenda kumtupa kilomita kama 2 katikati ya shamba la mazao.
Akiwa yuko kwenye takataka na matope alihisi maumivu makali na alipofumbua macho aligundua kuwa haoni.
Zilifanyika juhudi za kumfanyia upasuaji mara tatu, ila alipofikisha umri wa mika 12 ilibainika kwamba hatoona tena hivyo akawa kipofu rasmi.
Alipelekwa akaishi kwenye makazi ya vipofu katika mji wa Zamun, mpaka alipofikisha umri wa miaka 18, ilipomlazimu kurudi nyumbani kuwalea wadogo zake baada ya mama yake wa kambo kufariki.
Hiki ndicho kipindi ambacho alianza tokewa na mambo ya ajabu kama kuota ndoto za ajabu, kupata maono, kuskia sauti, kuongea na watu waliokufa na mimea.
Pia alianza kutabiri matukio ambayo yalitokea kwa usahihi kabisa.
Ndipo jina la Baba Vanga likaibuka likiwa na maana Bibi Vanga katika lugha ya wa Bulgaria.
Alifariki tarehe 11 mwezi 11 mwaka 1996, na kabla ya kifo chake alisema kuwa kutatokea binti huko Ufaransa ambaye akiwa na miaka 10 ataanza kuwa mtabiri kama yeye.
Ametabiri matukio mengi yaliyotokea iliwemo kuibuka kwa ISIS, sept 11, kifo cha Stalin, Princess Diana kuza nyambizi ya Kirusi alitabiri hadi kwa jina ila mimi hapa chini nitaandika ambayo hayajatokea atakayependa kuona mengine akagoogle.
2016-
Waislamu wataivamia Ulaya na kufanya Uaribifu mkubwa kwa miaka mingi itakayofuata.
2018-
China itakuwa taifa lenye uchumi na ushawishi mkubwa duniani
2028-
Binadamu wataweza kwenda sayari ya Venus, pia kutatengenezwa chanzo kipya cha nishati tofauti na vyanzo vya sasa
2033-
Barafu zipatikanazo kwenye pembe za dunia zitayeyuka kwa kiwango cha juu na kusababisha bahari kuongezeka ukubwa kwa kula eneo la nchi kavu
2033-2046
Uchumi wa dunia utakuwa kwa kiwango cha juu, na Ulaya kutasimikwa utawala wa Kislamu.

Kufikia 2046, binadamu ataweza kufyatua (clone) viungo na hivyo kuwa na uwezo wa kutengeneza kiungo chochote katika mwili wa binadamu
2066-
USA itashambulia utawala wa Kislamu katika nchi za Ulaya kwa kutumia silaha mpya ya hali ya hewa itakayosababisha ubaridi wa kugandisha vitu hapo hapo.
2076-
Madaraja baina ya binadamu yatakuwa yamekoma na Ujamaa kupotea kabisa duniani.
2084-
Mfumo wa tabia nchi utajirekebisha na kujirudisha kama ulivyokuwa awali kabla ya uharibifu
2088-2097
Utaibuka ugonjwa mpya, ambapo binafamu anazeeka kwa kasi na dawa yake itapatikana 2097
2100-
Kutokana na jua letu kupungua nguvu, hivyo binadamu atatengeneza jua litakalo mulika upande wa dunia ambao utakuwa umekosa nishati ya hili jua

2100-2130
Binadamu watakuwa kama maroboti, na mwaka 2025, nchi ya Hungary itapokea ishara toka kwa viumbe wa anga za juu.
Kufikia 2130, viumbe hao watatembelea dunia na kusaidia binadamu kujenga makazi chini ya bahari.

2164-2200
Wanasayansi watafanikiwa kubadili wanyama kuwa nusu binadamu.
Kufikia 2170, kutatokea janga la ukame litakalosababisha njaa.


2183, moja wapo la koloni lililoanzishwa na binafamu huko sayari ya Mars, litakuwa na uwezo mkubwa wa siraha za Nyuklia hivyo kudai uhuru wake kutoka duniani.
2189, milipuko mikubwa miwili ya Volkano itazuiwa na mwaka 2195 binadamu watakaokuwa wameanzisha makazi chini ya bahari watakuwa wameweza kujitegemea kwa kila kitu hawatahitaji msaada wa aina yoyote toka juu au nchi kavu.
2200-2300
Sayari zitabadili njia zake za kuzunguka jua (orbits)
Kutaibuka binadamu wapya ambao watakuwa mchanganyiko wa weusi, weupe na njano.
Pia binadamu ataweza pata nishati kutoka katika vacccum (kiswahili chake sijui ila ni sehemu isiyo na hewa) na black holes(ni sehemu katika ulimwengu ambayo ina nguvu ya uvutano mkubwa kiasi kwamba kila kinachoingia hakiwezi kutoka hata mwanga. Hutokea pale nyota itapokufa na kugandamizwa)
Pia mawasiliano mapya yananzishwa na viumbe wengine wa anga za juu na binadamu atakuwa anauwezo wa kusafiri kwa kurudi miaka ya nyuma.

2300, jua litapoa na kushindwa kutoa nishati kabisa hivyo binadamu atatengeneza majua mengine kwa ajili ya nishati.
Pia sheria, kanuni na siri nyingi za ulimwengu zitajulikana.
Ajali itasababishwa na jua lililotengenezwa na mwanadamu na kuleta maafa ya ukame na njaa kali.
2480-
Majua mawili yaliyotengenezwa na mwanadamu yatagongana na kuiacha dunia katika giza totoro.

3000-4000
Vita kali itaibuka baina ya binadamu watakaokuwa wanaishi kwenye sayari ya Mars.

Jiwe kubwa litagonga mwezi na kusababisha vipande vya miamba kutengeneza pete itakayokuwa imezumguka dunia kama ilivyo kwenye sayari ya Saturn. ( japo kwa Saturn ile siyo miamba ni barafu)
Hili litayokea miaka 10 kabla ya kuanza kwa zama mpya.

3797-
Dunia itakuwa imeharibiwa vibaya kiasi cha kutokalika, ila binadamu watakuwa na uwezo wa kuishi katika sayari mbalimbali.
3800-
Binadamu wataamia kwa wingi katika sayari moja ambapo hali ya heea haitokuwa nzuri kwa ustawi wa viumbe wengine hivyo kutakuwa na mapigano ya kugombea rasilimali na nusu ya wakazi wa sayari hiyo watakufa kwenye hiyo vita.
Kufikia 3815, vita itaisha, maendeleo na ustaarabu utakoma na binadamu wataishi kama wanyama
3871-
Atatokea nabii mpya, atakayewahubiria watu kuhusu kutenda mema na kuhusu dini.
Watu wote watamuunga mkono na ataanzisha dini moja kwa watu wote.
3878, huyo nabii atawafunza kuhusu sayansi iliyosahauliwa.

4000-5000
Baada ya kuanza kwa zama mpya, miji mipya itajengwa na kutakuwepo maendeleo ya kisayansi.

4304, hakuna ugonjwa utakaokuwa hauna tiba
4308, binadamu watakuwa na uwezo wa kutumia 34% ya ubongo wao. Uovu na chuki itapotea baina ya binadamu.
4509, binadamu watamjua sana Mungu na watakuwa na uwezo wa kuwasiliana naye moja kwa moja.
4599, binadamu atakuwa na uwezo wa kuishi bila kufa.
4674, maendeleo yatakuwa yamefika kwenye kilele cha juu kabisa na kutakuwa na idadi ya watu bilion 340 walisambaa katika sayari mbali mbali.
Baada ya mwaka 5000, binadamu watakuwa wamefanya uamuzi wa kuvuka mipaka ya ulimwengu huu ambapo 60% watakubari na 40% hawatakataa.
5079, ulimwengu utafika kikomo.
11 March 2019
10 March 2019
VIONGOZI WALIOWAHI KUONJA MADARAKA KWA MUDA MFUPI MNO
John F Kennedy JFK anafahamika kama miongoni mwa marais wa Marekani waliokaa madarakani muda mchache zaidi
Sasa leo tunawajadili viongozi waliokaa madarakani(walioyatumikia madaraka) kwa muda mchache zaidi
Kati yao hakuna aliyefikisha hata kawiki kaamoja akiyatumikia hayo madaraka aliyoyapata/pewa
Hapa kuna Wafalme,mawaziri wakuu n.k
--------------------------------------------------------------------
10.Sultan Khalid Bin Bargash

Huyu alikuwa Sultani wa Zanzibar mnamo mwaka 1869 baada ya kifo cha binamu yake lakini akaonja madaraka kwa siku mbili tu
Waingereza baada ya kusikia Bargash kawa kiongozi wa Zanzibar walimpa masaa 24 aachie madaraka kwa hiyari yake sababu hakuwa chaguo lao, lakini akawagomea na kupelekea baada ya siku moja kupita Waingereza watume meli zao za kivita na wanajeshi
Hapo ndo ikazaliwa vita iliyojulikana kama Anglo Zanzibar War ambayo ilidumu kwa muda wa dk 38 pekee iliyoisha August 27 1869 na kuwa Vita fupi zaidi kuwahi kutokea duniani
Wakati wa vita hiyo wazanzibar waliokufa na kujeruhiwa ni 500 wakati mwingereza aliyeumia ni mmoja pekee, boti mbili zilizama
Hivyo jamaa huyu sultan alitawala Zanzibar kwa muda wa siku 2 tu
9.Diasdado Cabello
Alizaliwa April 1963
Huyu bwana alionja Urais wa Venezuela kwa muda wa siku moja pekee baada ya Rais kujiuzulu kufuatiia kuonekana anasapoti ubepari
Hivyo Cabello akachukua madaraka kisha akamchagua Hugo Chavez kuwa Makamu wake wa rais halafu yeye mwenyewe akajiuzulu na Chavez kuwa Rais..
.Mchezo ndo ulivyochezwa na kuisha kijanjajanja tu
Yaani kautumikia urais kwa muda wa siku moja pekee hata gwaride hakukagua
Waingereza baada ya kusikia Bargash kawa kiongozi wa Zanzibar walimpa masaa 24 aachie madaraka kwa hiyari yake sababu hakuwa chaguo lao, lakini akawagomea na kupelekea baada ya siku moja kupita Waingereza watume meli zao za kivita na wanajeshi
Hapo ndo ikazaliwa vita iliyojulikana kama Anglo Zanzibar War ambayo ilidumu kwa muda wa dk 38 pekee iliyoisha August 27 1869 na kuwa Vita fupi zaidi kuwahi kutokea duniani
Wakati wa vita hiyo wazanzibar waliokufa na kujeruhiwa ni 500 wakati mwingereza aliyeumia ni mmoja pekee, boti mbili zilizama
Hivyo jamaa huyu sultan alitawala Zanzibar kwa muda wa siku 2 tu
9.Diasdado Cabello
Alizaliwa April 1963
Huyu bwana alionja Urais wa Venezuela kwa muda wa siku moja pekee baada ya Rais kujiuzulu kufuatiia kuonekana anasapoti ubepari
Hivyo Cabello akachukua madaraka kisha akamchagua Hugo Chavez kuwa Makamu wake wa rais halafu yeye mwenyewe akajiuzulu na Chavez kuwa Rais..
.Mchezo ndo ulivyochezwa na kuisha kijanjajanja tu
Yaani kautumikia urais kwa muda wa siku moja pekee hata gwaride hakukagua
8.Ratu Tevita Momoedomu

Alizaliwa Januari 13 mwaka 1946Huyu jamaa alikuwa Waziri mkuu wa Fiji katika muhula/vipindi viwili vifupifupi kama stuli za Tandale pale Manzese..
Mwaka 2000 alikaa madarakani kwa muda wa masaa mawili pekee wakati mwaka 2001 alikaa madarakani kwa siku mbili tu
Mnamo mwaka 2000 yalitokea mapinduzi/maasi ambapo yeye pekee akajikuta ndo amebaki kwenye jengo la serikali hivyo kuwa kiongozi kulingana na katiba ya nchi hiyo .....yaani kama ngekewa vile halafu mwaka 2001 akachaguliwa tena baada ya kuachia madaraka ili kukidhi matakwa ya kikatiba7.Roger LaFontant

Alizaliwa mwaka 1931 na kufariki dunia 1991 akiwa na umri wa miaka 60Huyu alikuwa kiongozi wa kijeshi huko Haiti ambapo mwaka 1991 alikuwa Rais kwa masaa 24 tu
Kisura anafanana na mchungaji Mtikila
Rais alijiuzulu hivyo Katiba ya nchi hiyo kumpa madaraka Jaji Mkuu Estha Pascal Trouillot ambaye aliitisha uchaguzi wa kidemokrasia
Lakini bwana mkubwa Fountant akatumia fursa hiyo kufanya mapinduzi na kujitangazia Urais
Ghafla bin vuuuu wajanja zaidi yake wakampindua ndani ya masaa 24 tu yaani wakati anaamka tu huko Ikulu akijiadaa kupiga mswaki hata swimming pool hakugusa
Alikuwa rais kwa masaa 24 pekee6.Joseph Goebbels

Alizaliwa mnamo mwaka 1897 na kujiua mwaka 1945 akiwa na umri wa miaka 47 Huyu alikuwa Kansela wa Ujerumani kwa muda wa masaa 5 pekee mwaka 1945 May 1
Wakati Vita Kuu ya Pili ikiendelea na Adolf Hitler kuonekana kuzidiwa akaamua kumteua swahiba wake Goebbels kuwa Kansela akiamini ni Waziri wa Propaganda ndo pekee anayeweza kumuokoa jahazi lake linalozama.
Lakini hata kabla hawajaanza propaganda zao za Hamphrey Polepole wakagundua wamezingirwa hivyo kuamua kujiua
Kuna badharia nyingi kuhusu kifo chake pamoja na cha Adolf Hitler
Jamaa kaonja ukansela masaa yasiyozidi matano pekee5.Boris Yeltsin



Alizaliwa mnamo mwaka 1931 na kufariki dunia 2007 akiwa na umri wa miaka 76 baada ya kupambana na maradhi kwa kipindi kirefu
Huyu mzee alijiteua mwenyewe kuwa Waziri mkuu wa Urusi mnamo mwaka 1998.
Hii ilikuwa wakati yeye akiwa Rais na mgogoro wa kisiasa ukiwa umepamba moto hivyo akaamua kumpunguzia majukumu Waziri Mkuu kwa kujiteua yeye mwenyewe
Baada ya kukosolewa vikali na wananchi wake na wapinzani na kuambiwa ni dikteta na mzee wa kukurupuka kama yule wa Chato akaamua fasta kuachia huo Uwaziri mkuu na kumteua mtu mwingine
Yaani alikuwa Waziri mkuu ndani ya masaa manne tu...kukurupuka ni kubaya!4.Skender Gjinushi
Huyu mzee alijiteua mwenyewe kuwa Waziri mkuu wa Urusi mnamo mwaka 1998.
Hii ilikuwa wakati yeye akiwa Rais na mgogoro wa kisiasa ukiwa umepamba moto hivyo akaamua kumpunguzia majukumu Waziri Mkuu kwa kujiteua yeye mwenyewe
Baada ya kukosolewa vikali na wananchi wake na wapinzani na kuambiwa ni dikteta na mzee wa kukurupuka kama yule wa Chato akaamua fasta kuachia huo Uwaziri mkuu na kumteua mtu mwingine
Yaani alikuwa Waziri mkuu ndani ya masaa manne tu...kukurupuka ni kubaya!4.Skender Gjinushi


Alizaliwa Disemba 24 mwaka 1949
Huyu alionja Urais wa nchi ya Albania kwa muda kiduchu kama masaa mawili au manne tu
Ilikuwa mwaka 1997 baada ya uongozi wa kibepari wa Sali Berisha kushindwa uchaguzi wa kidemokrasia halafu kukataa kuachia madaraka hivyo Spika Slender akaamua kuchukua madaraka kwa mujibu wa katiba kuwa Rais wa mpito
Kisha Bunge la Albania likaamua kumtangaza mshindi halali wa Uchaguzi Mkuu Rexhep Meidani kuwa Rais mpya wa Albania
Hii ilifanyika ndani ya masaa manne pekee3.Carlos Manuel Piedra
Huyu alionja Urais wa nchi ya Albania kwa muda kiduchu kama masaa mawili au manne tu
Ilikuwa mwaka 1997 baada ya uongozi wa kibepari wa Sali Berisha kushindwa uchaguzi wa kidemokrasia halafu kukataa kuachia madaraka hivyo Spika Slender akaamua kuchukua madaraka kwa mujibu wa katiba kuwa Rais wa mpito
Kisha Bunge la Albania likaamua kumtangaza mshindi halali wa Uchaguzi Mkuu Rexhep Meidani kuwa Rais mpya wa Albania
Hii ilifanyika ndani ya masaa manne pekee3.Carlos Manuel Piedra

Alizaliwa mnamo mwaka 1895 na kufariki dunia 1988 akiwa na miaka 93
Huyu alikuwa Rais wa mpito kwa muda kati ya masaa 2 hadi 5 baada ya kujiuzul ;Fulgencio Battista mwaka 1959.
Hii ilikuwa baada ya Makamu wa Rais naye kuingia mitini kufuatia mapinduzi yaliyoongozwa na vijana matata akina Fidel Castro, Camilo Confuegos n.k
Katiba ilikuwa ikimraka Jaji Mkuu mwenye umri mkubwa zaidi ndo achukue madaraka hivyo Piedra akatangazwa Rais mpya halafu fasta ndani ya nasaa machache akina Castro walikuwa washaiteka Havana hivyo akakimbilia Ubalozi wa Marekani na akina Castro kuchukua madaraka
Yaani alidumu kati ya masaa mawili au manne tu2.Siaka Stevens


Alizaliwa mwaka 1905 na kufariki dunia mwaka 1988 akiwa na umri wa miaka 82.....
Aliwai kuwa Rais wa Sierra Leone kuanzia mwaka 1971 hadi mwaka 1985
Huyu alikuwa Waziri Mkuu wa Sierra Leone mnamo March 21 mwaka 1967 aliapishwa kuongoza Taifa hilo
Lakini ndani ya nusu saa tu waasi wakamzingira na kumkamata hivyo kuwa nwiaho wa utawala wake wa kiKassimu Majaliwa
Baadaye akafanikiwa kurudi madarakani kuanzia mwaka 1968
Yaani alitawala nusu saa tu mwaka 1967 kama Waziri Mkuu1.Prince Luis Felipe

Kama mnavyojua utawala wa kifalme mrithi hujulikana mapema hata kabla ya kifo cha Mfalme
Sasa mwaka 1908 Mfalme Carlos wa Ureno aliuawa papo hapo wakati wa ziara ya kifalme ambapo pia mwanawe Luis Felipe alijeruhiwa
Sasa wakati anawahishwa hospitali tayari alitambulika km Mfalme mpya wa Ureno japo alikuwa bado hajavalishwa taji rasmi...ndani ya dakika 30 akafariki dunua akiwa njiani kupelekwa hispitali kutokana na kupoteza damu nyingi
Yaani mwanamfalme alikuwa Mfalme kwa nusu saa pekee
..........................MWISHO..........................
Sasa mwaka 1908 Mfalme Carlos wa Ureno aliuawa papo hapo wakati wa ziara ya kifalme ambapo pia mwanawe Luis Felipe alijeruhiwa
Sasa wakati anawahishwa hospitali tayari alitambulika km Mfalme mpya wa Ureno japo alikuwa bado hajavalishwa taji rasmi...ndani ya dakika 30 akafariki dunua akiwa njiani kupelekwa hispitali kutokana na kupoteza damu nyingi
Yaani mwanamfalme alikuwa Mfalme kwa nusu saa pekee
..........................MWISHO..........................
Subscribe to:
Comments (Atom)


